MUNIRA AFISA MIKOPO SEHEMU YA 6

 


SEHEMU YA 06

Kesho yake asubuhi nilienda kazini vizuri tu, nilipofika kazini nilimkuta Meshack akiwa amekaa ofisini kwake, ameshafika mapema tu, nikamuita


“Mr Mushi”


Akaniambia “Naam”


“Ina maana umeshafika asubuhi yote hii?”


“Ah, nimelala nawaza tu ile pesa iliyopotea, usingizi hakuna, natamani tufunge tu hii ofisi kwa kweli” aliniambia


“I am sorry my boss….sikujua kama itakuathiri vile, naomba uwe mvumilivu everything will be okay, sawa?”


“Daah, anyway, leo utakuwa wapi jioni, nataka tutoke kidogo tukapunguze stress”


“Mi niko free for you anytime ukiwa unanihitaji niambie tu boss”


“Okay basi saa moja tukutane”


“Wapi?”


“Masaki” aliniambia


“Okay”


*

Niliendelea kufanya kazi kwa bidii sana siku ile, kwa sababu jana yake niliacha viporo vingi sana, nikiwa nafanya kazi ndani mara Kevin aliingia ofisini kwangu na kuniuliza

“Sister vipi”


“Poa vipi?” nilimuuliza


“Fresh, kuna mtu anakutafuta hapo nje”


“Mtu gani?”


“Nenda kamsikilize amesema hawezi kuja ndani”


“Ni nani huyo?”


“Simfahamu”


“Ah” nilisema huku nikiinuka na kutoka nje niende nikamuone, nilipofika nje nilikuta gari kali imeegesha mbele ya ofisi yetu, nilipotazama niliona mkono unaniita kupitia kwenye kioo cha gari lile.


Nilishtuka kidogo maana sikujua ni nani ambaye ana gari zuri namna ile, mimi sikuwa na rafiki mwenye gari ya aina ile, nikajua labda ni mtu anataka kuniona kikazi.


Nikasogea kwenda kumtazama ni nani, nilipofika sikuamini, Rayan huyu hapa, na yupo peke yake, nikashtuka sana na kumuuliza


“Vipi tena?”


“Aaaamh sorry nimekuja bila taarifa lakini nilijua hapa nitakukuta” aliniambia


“Rayan, unanitafuta nini? Unataka kufungwaa?” nilimuuliza


Rayan alitabasamu halafu akaniambia “Sorry, lakini kwani nilikukwaza nini hadi ukaniblock jana?? Mbona unanifanyia hivi?” aliniuliza


“Usilete ujinga wako kwangu naomba uondoke”


“Nimeambiwa jina lako unaitwa Munira, kiukweli jina ni zuri kama wewe, nimefurahi sana kulijua, wewe ni mzuri kama jina lako, bado ninahitaji kampani yako” aliniambia


“Naomba uondoke”


“Munira ninakupenda” aliniambia


“We vipi? Unanipendaje mtu hunijui sikujui bana mbona nyenyenye nyingi….embu niache”


“Nielewe Munira, naomba tuwe wote ikiwezekana panda gari tuondoke zetu”


“We” nilisema kwa hasira huku nikimnyooshea kidole “Nisikilize kwa makini, niachie upumbavu wako….mimi hapa kazini boss ni mwanaume wangu, anapokuja kukuona hapa unaniletea matatizo sitaki kujiharibia kazi, wala mahusiano yangu, nina malengo naye”


“Ok ninaondoka lakini please nenda kanitoe kwenye blacklist, ninahitaji kuongea na wewe nina surprise yako” aliniambia


“Surprise ya nini? Ninaomba usinizo….” Kabla sijamaliza sentensi nilisikia sauti ya boss akiniita ndani “Nenda zako boss ananiita” nilisema huku nikigeuka naondoka zangu lakini akaniita na kuniambia


“Usisahau kunitoa blacklist…..” alisema “Halafu shika hii” alisema nikamgeukia nikamuona amechukua bahasha ya kaki ndogo iliyokuwa na kitu ndani akaniambia “Itakusaidia kupunguza deni lako hilo halafu tutawasiliana”


Nilirudi hatua mbili na kupokea ile bahasha, nilipochungulia ndani, kibunda cha noti za elfu kumi kumi hiki hapa….nilimshangaa kwanza, na sijui alileta za nini, nikamuuliza “Hizi za nini?”


“Tutawasiliana” alisema halafu akawasha gari akateleza……………JE UNAFIKIRI MUNIRA ATACHOMOA KWA HII NJEMBA?? NA JE HII NJEMBA INAMUIGIZIA KWAMBA INA PESA AU INAZO KWELI? USIKOSEE SEHEMU YA 07


GUSA HAPA KUSOMA SEHEMU YA SABA (7)





Chapisha Maoni

Join Our
Whatsapp Group